banner

Wednesday, May 28, 2014

Tanzania yadai kuwa Waasi wa M23 walitoka Rwanda

Tanzania kwa mara ya Kwanza imesema inayo uhakika kuwa waasi wa M23 walioondolewa nchini Jamuhuri ya Kongo  ni raia Rwanda. Waziri wa Mambo ya Nje Benard Membe ameliambia Bunge la Tanzania kuwa anao uhakika kuwa waasi   wa  M23 walitokea nchini Rwanda.
 
Hii ni Mara kwanza kwa Tanzania kukiri hadharani kuwa inao uhakika kuwa waasi hao ni raia wa Rwanda.
 
Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimepeleka majeshi Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambayo kwa kushirikiana na yale ya umoja wa Mataifa yaliwaondoa waasi hao DRC

Waasi wa M23
Waasi wa M23

Matamshi hayo ya Waziri huyo aliyatoa wakati alipokuwa akiwasilisha hotuba ya Bajeti ya Wizara yake ambapo pia alikiri kuwa bado uhusiano wa Tanzania na Rwanda sio mzuri.Hata hivyo upande wa Upinzani ulishambulia Waziri Membe  ukidai kwamba Waziri huyo anachochea kuvurugika kwa uhusiano wa Watanzania na Rwanda kwa kuhisi kuwa M23 ni Wanyarwanda nahata kutaka achukuliwe adhabu kali.

Mbali na tuhuma hizo Waziri Membe alizidi kusisitiza kuwa waasi wa M23 ni raia wa Rwanda akisema hiyo ni ripoti ya Umoja wa Mataifa.

Mbali na waziri,  baadhi ya wabunge walimuunga mkono waziri Membe kuwa waasi wa M23 ni raia wa Rwanda.

Socializer Widget By Blogger Yard
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →

0 comments:

Post a Comment