banner

Wednesday, April 23, 2014

Mwanafunzi akutwa amekufa kisiwani Pemba

 MAMIA ya wananchi wa shehia za Wawi, Wara na wapita njia wengine, jana wameshuhudia mwili wa marehemu

MOHAMMED Soud Makame (17), ambae ni mwanafunzi wa kidato cha pili katika skuli ya sekondari Vikunguni, amekutwa amekufa ndani ya nyumba iliyokuwa haijahamiwa katika mtaa wa  Wawi wilaya ya Chake Chake Pemba.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, taatifa za tukio hilo zilitolewa na mtoto mmoja ambae aliukuta mwili huo ndani ya nyumba hiyo, wakati yeye alipokuwa akifukuza kuku.

Walisema baada ya kuuta mwili huo, waliamua kutoa taarifa kwa vyombo husika ikiwa ni pamoja na polisi, hospitali, sheha wa shehia ya Wawi na baadhi yao kupiga simu kwa waandishi wa habari juu tukio hilo.

Walisema waalimkuta marehemu akiwa na kitambaa ambacho wakati wa uhai wake alikuwa akikivaa kichwani, ingawa kwa jana walikikuta kikiwa shingoni mwake, mithili ya mtu aliejitia kitanzi.

Socializer Widget By Blogger Yard
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →

0 comments:

Post a Comment