banner

Thursday, April 17, 2014

UKAWA wamegoma kabisa kuhudhuria mkutano wa bunge maalum la katiba


 Umoja wa katiba ya wananchi bungeni -UKAWA- umegoma kabisa kuhudhuria mkutano wa bunge maalum baada ya kutoka katika mkutano uliofanyika Aprili 16 kwa madai ya mkutano huo kugubikwa na matusi, kashfa na vitisho vinavyofanywa na baadhi ya viongozi kwa wananchi.

Akizungumzia masikitiko yake mwenyekiti wa kamati ya bunge maalum, Mhe. Samweli Sita amesema licha ya bunge hilo kumwita bungeni Mhe. William Lukuvi kutoa ufafanuzi wa tuhuma  zinazomkabili  ameutaka UKAWA  kuja katika kamati ya uongozi kueleza kwa undani nini hatma ya maamuzi yao.

Akiitikia wito wa kuitwa bunge hilo,waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera uratibu na bunge, Mhe. William Lukuvi ameeleza hofu yake kuhusu muundo wa serikali tatu  na kulieleza bunge dhamira ya vyama vikuu vya upinzani vya kugawana Tanganyika na Zanzibar.

Wakitoa maoni yao nje ya bunge, baadhi ya wabunge wameutaka umoja huo kuitikia wito wa wenyekiti wa bunge hilo wa kuhudhuria mikutano kama kawaida na kupeleka malalamiko yao kwa kamati ya uongozi ili kutafuta njia bora ya kufikia mwafaka na kuwapatika wananchi katiba mpya.

ITV imeutafuta uongozi umoja wa katiba ya wananchi-UKAWA uliokuwa ukifanya mkutano wake wa ndani na kuzungumza na mwenyekiti wa umoja huo Mhe Freeman Mbowe ambae amepinga kauli ya kiongozi huyo wa serikali kudai kuwa ni hofu yake binafsi na kusisitiza baadhi ya vinongozi wengine wameshawahi kutoa kauli kama hiyo ambapo ametoa msimamo wa umoja huo.


Credit: ITV

Socializer Widget By Blogger Yard
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →

0 comments:

Post a Comment