banner

Sunday, April 13, 2014

Mzee Gurumo afariki dunia.....

 

Mkongwe wa Dansi nchini, Maalim Muhidin Gurumo aliyekuwa akitumikia Bendi ya Msondo Ngoma ‘Baba ya Muziki’ kabla ya kustaafu mwaka jana, amefariki  dunia.

 Mwanamuziki huyo amefariki leo  alasiri  katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa amelazwa kwa matibabu.

Mzee  Gurumo  amefariki  dunia  baada  ya  kusumbuliwa  na  maradhi  kwa  muda  mrefu, hali  iliyomfanya  astaafu  muziki....

Msiba  upo  nyumbani  kwa  marehemu  Tabata  Makuburi  na  mipango  yote  ya  mazishi  itafanyika  hapo.....

Mungu  ailaze  Roho  ya  marehemu  mahali  pema  peponi-Amina

Socializer Widget By Blogger Yard
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →

0 comments:

Post a Comment