banner

Wednesday, April 16, 2014

Mzazi matatani kwa wizi wa mtoto wa Siku 5 huko Mbeya..!!

 
MAMA MZAZI WA MTOTO ALIYEIBIWA
BABA MZAZI ANAYETUHUMIWA KWA WIZI WA MTOTO

Jeshi la Polisi linamshikilia Salehe Issah Mwangosi(29) Mkazi wa Tankini Kasumulu Kata ya Itope Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya kwa tuhuma za wizi wa mtoto jinsi ya kiume mwenye umri wa  siku sita.
 
Imedaiwa kutenda kosa hilo dhidi ya mzazi mwenzake aliyefahamika kwa jina la Mboka Mwakikagile(21)mkazi wa Kitongoji cha Sama A Kijiji cha Ibanda Kata ya Itope Jumapili April 6 mwaka huu majira ya saa nne asubuhi kwa kushirikiana na mwanamke mmoja ambaye hajafahamika jina mara moja aliyejifanya ni mama yake mkubwa wa mtuhumiwa.
 
Mipango hiyo iliyoanza kuandaliwa na mtuhumiwa siku tatu baada ya mtoto kuzaliwa kwa kutumia simu ya kiganjani ya mtuhumiwa yenye namba 0767356222 na mzazi wa mtoto kwa namba 0757006839 ambapo siku ya tukio Salehe alimwambia kuwa mama yake mkubwa angekwenda kumjulia hali mtoto aliyezaliwa.
 
Baada ya Salehe kuwasiliana na mzazi mwenzake walikubaliana Mama yake mkubwa angekwenda Jumapili Aprili 6 mwaka huu majira ya saa nne asubuhi ambapo mwanamke huyo alifika nyumbani kwa Mboka(Mzazi wa mtoto)ambapo aliwakuta wazazi wake akiwemo Mzee Lupalo Elija Mwakikagile(90) na mkewe Nelly Kyusa(49) ambao walimpokea.
 
Mwanamke huyo alifikanyumbani kwa Mwakikagile akiwa ameshika mkoba wenye nguo za mtoto mchanga,sabuni na mahitaji mengine ambapo alijieleza kuwa yeye ni afisa wa Mamlaka ya mapato na Mama mkubwa wa Salehe hivyo amekuja kwa ajili ya kumjulia hali na kumpa pole Mboka kwa kujifungua.
 
Mama huyo baada ya kumwangalia Mtoto alidai ana matatizo ya macho hivyo waende naye Zahanati ya Njisi Kasumulu kwa ajili ya matibabu

Socializer Widget By Blogger Yard
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →

0 comments:

Post a Comment