banner

Tuesday, May 20, 2014

UKAWA wapata Pigo Jingine mkoani Simiyu....Wananchi wawapokea kwa Mabango ya kuwataka warudi bungenii kujadili matatizo yao na si muundo wa Serikali


Umoja  wa  katiba  ya  wananchi ( UKAWA ) , juzi  wamepokelewa  kwa  mabango  katika  wilaya  ya  Bariadi, mkoani  Simiyu  yaliyowataka  warudi  bungeni  kabla  ya  kuanza  mkutano  wao  kwenye  uwanja  wa  michezo  wa   Halmashauri  ya  mji  huo  ambao  ulihudhuriwa  na  watu  wachache.....

Mabango  hayo  yalikuwa  na  ujumbe  uliowataka  wajumbe  wa  umoja  huo  kurudi  bungeni  kujadili  rasimu  ya  pili  ya  katiba  ili  kushindana  kwa  hoja  na  wajumbe  wa  bunge  hilo  weye  mtazamo  tofauti  na  wao....

Ujumbe  wa  Umoja  huo  ulioongozwa  na  mwenyekiti  wa  vijana  chama  cha  demokrasia  na  maendeleo  ( BAVICHA ) taifa, Bw. John Heche  ulishangaa  kuona  mabango  hayo  na  mahudhurio  ambayo  hawakuyatarajia  licha  ya  mkutano  huo  kutangazwa  siku  mbili  katika  mji  mzima....

Wakiwa  wamebeba  mabango  hayo, wananchi  hao  waliutaka  ujumbe  huo  kuwashawishi  wajumbe  waliosusia  vikao  vya  bunge  warudi  bungeni  ili  kujadili  matatizo  ya  watanzania  na  si  muundo  wa  serikali....
"Sisi  hatuna  haja    na    muundo  wa  serikali  hata  zikiwa  10 , mbili  au  3, tunataka  kunufaika  na  pamba,bei  iongezeke, tupate  pembejeo  za  kutosha  na  kupewa  matrekta  ili  tuweze  kunufaika," alisema  Bw. Mugata Munghu.

Wakazi  wengine  walioshiriki  mkutano  huo  walidai  asilimia  kubwa  ya  wakazi  wa  mkoa  huo  ni  wakulima  na  wafugaji  ambapo  changamoto  kubwa  waliyo  nayo  ni  ukosefu  wa  maeneo  ya  kufanyia  uzalishaji....

"Hatuna  maeneo ya  kulishia  mifugo  yetu  na  kufanya  shughuli  za  kilimo,rudini  bungeni  mkatutetee  tupate  maeneo  ya  kutosha  kwa  ajili  ya  wafugaji  na  wakulima, tunataka  kuachana  na  mapigano  ya  kila  siku, wekeni  sheria  ya  kuilazimisha  serikali  itenge  maeneo  haya, hatuoni  umuhimu  wa  nyie  kutanga taga  nchi  nzima  kutaka  serikali  tatu," alisema  Bw. John Matale

Viongozi  wa  umoja  huo  waliendelea  kuhutubia  mkutano  huo  mbali  ya  kuwepo  kelele  za  vijana  waliokuwa  wakizunguka  na  mabango  huku  viongozi  hao  wa UKAWA  wakitumia  muda  mwingi  kumshambulia  katibu  mkuu  wa  CCM,Abdulrahman  Kinana.

Socializer Widget By Blogger Yard
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →

0 comments:

Post a Comment