banner

Sunday, May 25, 2014

PINDA asisitiza kuwa Serikali ya Tanzania Haiwezi kuwa na Dini

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda (pichani) amesema Serikali itaendelea kusimamia msimamo wake wa kutokuwa na dini wala nchi kutokuwa na dini lakini itaendelea kuruhusu watu wawe na dini zao.
 
Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumapili, Mei 25, 2014) kwenye ibada ya kumuweka wakfu Askofu Mteule Conrad Nguvumali wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Rukwa iliyofanyika kwenye Uwanja wa Nelson Mandela, mjini Sumbawanga.
 Waziri Mkuu ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Rais Jakaya Kikwete ambaye yuko nje ya nchi kikazi, alisema: 
 
“Leo tukiruhusu Serikali iwe na dini na tayari katika dini zote kuna makundi madogo madogo, je wale wa upande mwingine utawaacha wapi?”.
 
 Pia alitumia fursa hiyo kuwaasa viongozi wa dini nao pia waangalie wasitumbikie kwenye mtego wa siasa na kuruhusu kanisa zima liwe la chama fulani kwani miongoni mwa waumini wao wapo pia wapenzi wa vyama vingine.
 
 Pinda
 
“Kama mtu binafsi, kiongozi wa dini anaweza kuwa mpenzi wa chama lakini kama Kanisa tusiruhu hali hiyo,” alionya.
 Aliwaomba viongozi wa dini waendelee kuliombea Taifa na hasa waombee amani ya Taifa hili. “Ninawasishi viongozi wa dini msichoke kuombea amani ya Taifa hili kwani amani ikipotea kama nchi hatuna mahali pa kukimbilia.”

Socializer Widget By Blogger Yard
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →

0 comments:

Post a Comment