Katibu Mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif
Sharif Hamad akichukua fomu ya kugombea tena nafasi ya Katibu Mkuu wa
Chama hicho katika ofisi kuu za CUF Wilaya ya Magharibi Kilimahewa
Zanzibar. Anayemkabidhi ni Kaimu Katibu wa CUF Wilaya ya Magharibi Ussi
Juma Hassan.
Katibu Mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif
Sharif Hamad akionyesha fomu ya kugombea tena nafasi ya Katibu Mkuu wa
Chama hicho katika ofisi kuu za CUF Wilaya ya Magharibi Kilimahewa
Zanzibar.
Katibu Mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif
Sharif Hamad akizungumza na wanachama waliojitokeza kumsindikiza wakati
wa kuchukua fomu hiyo. katika ofisi kuu za CUF Wilaya ya Magharibi
Kilimahewa Zanzibar.
Katibu Mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif
Sharif Hamad akizungumza na waandashi wa habari katika ofisi kuu za
CUF Wilaya ya Magharibi Kilimahewa Zanzibar, baada ya kuchukua fomu ya
kugombea tena nafasi ya Katibu Mkuu wa Chama hicho (Picha na Salmin
Said, OMKR)
Na Hassan Hamad OMKR
Katibu
Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, leo
amechukua fomu ya kugombea tena nafasi ya Katibu Mkuu wa Chama hicho.
Maalim
Seif amechukua fomu hiyo katika Ofisi za CUF zilizopo Kilimahewa Wilaya
ya Magharibi Unguja, na kusindikizwa na viongozi na wanachama kadhaa
wakati akichukua fomu hiyo.
Akizungumza
na waandishi wa habari baada ya kuchukua fomu hiyo Mhe. Maalim Seif
ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar amesema ameamua
kuchukua fomu hiyo ili aendelee kuwatumikia wanachama na kufikia malengo
ya chama waliyojiwekea.
Amefahamisha
kuwa pia ameshawishika kuchukua fomu hiyo baada ya kujitokeza kauli za
kutaka kuzorotesha serikali ya umoja wa kitaifa.
Amesema akiwa kiongozi wa Chama ataendelea kuwatumikia wanachama na wananchi hadi pale chama kitakapotimiza malengo yake
0 comments:
Post a Comment