banner

Monday, May 26, 2014

Al Shabaab waua Wanajeshi wawili wa Kenya Somalia.

SERIKALI ya Kenya imethibitisha kuwa maofisa wake wawili wa jeshi wameuawa na wengine wawili kujeruhiwa, baada ya wapiganaji wa Kiislamu wa Al Shaabab kufanya shambulio la kuvizia, baada ya magari yao kukwama barabarani huko Somalia.

Ripoti zinasema msafara wa wanajeshi wa Kenya ulikuwa ukielekea eneo la Ras Kamboni wakati shambulio hilo lilipotokea. Kamanda wa polisi mjini Mombasa, Robert Kitur amethibitisha kuwa shambulio hilo limetokea. Kwa upande wao, msemaji wa Al shabaab, Abu Mus’ab amedai kuwa wapiganaji wake walifanikiwa kuteketeza magari kadhaa ya Jeshi la Kenya, madai ambayo yamekanushwa vikali na utawala wa nchi ya Kenya.

Al-Shabaab
Wapiganaji wa Kiislamu wa Al Shaabab.

Aidha amesema hata hivyo wapiganaji kadhaa wa Al Shabaab waliuawa na wengine kujeruhiwa wakati wa makabiliano hayo. -BBC

Socializer Widget By Blogger Yard
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →

0 comments:

Post a Comment